Friday, July 12, 2013

HAWA NDIO WANAUME WALIOTEMBEA NA BEYONCE KABLA YA JAY Z

jayz_beyonce
Beyonce mwanamke mrembo,wenye kipaji kikubwa na pia anaingiza pesa nyingi sana kwa kazi yake ya uimbaji na nyingine, bila shaka wanaume wengi wanamtamani wangekuwa na uhusiano naye au kumuoa kabisa kama Jay Z alivyofanya. Kwenye interview nyingi anazofanya Beyonce likija swali la kuzungumzia maisha yake ya kimapenzi huwa anasisitiza mwanaume wake wa kwanza kabisa aliyemtoa usichana wake ni Jay Z kitu ambacho watu wengi na waandishi hawakubaliani nacho. Hiyo yote ni kutokana na Beyonce kuwa na historia ya kuwa na uhusiano na wanaume wengine hapo zamani.Hii hapa list ya watu nane waliojaribu na waliowahi kuwa na mahusiano ya wazi au ya siri na Beyonce kabla ya kuwa na Jay Z.
beyonce-lyndell-1
Lyndell Locke, huyu jamaa ndiyo alikuwa mpenzi wa kwanza wa Beyonce. Unaambiwa jamaa alikuwa akimsindikiza Beyonce kwenye mazoezi ya kuimba na kucheza akiwa ndiyo yupo kwenye harakati za kuwa star. Beyonce anasisitiza kwamba pia hajawahi kuwa na uhusiano wa chumbani na huyu jamaa.
camron-4
Cam’Ron, msanii maarufu aliyewahi kutamba na ngoma Oh Boy, alisema kwamba kwasababu walifanya ngoma pamoja na Beyonce na katika mambo yao mengine huko nyuma ya pazia. Beyonce alimpa nafasi ya ku-share chumba kimoja na yeye lakini watu wengi hawaya amini maneno ya Cam’Ron.
justin-timberlake-55th-annual-grammy-awards-02
Justin Timberlake, moja ya marafiki wakubwa wa mume wa Beyonce. Kulikuwa na uvumi kwamba wawili hawa Justin na Beyonce wali-spend usiku mmoja kwenye club na baadaye kufanya vitu vingi. Japokuwa hii habari haikuwa na uthibitisho wowote lakini ilivuma kwa wakati wake.
michael_jackson
Michael Jackson, baada ya Michael Jackson kufariki P.Diddy alitoa story kwamba kuna siku MJ alitaka kwenda kwenye party pamoja na Diddy akiwa na lengo kubwa la kutaka kukutana na Beyonce na kumelezea hisia zake. Duh! Kumbe Michael Jackson sio mkali wa kuchagua style za kucheza na melody tu, hadi wanawake wazuri anajua kuchagua.
mosdef
Mos Def alijaribu kumpata Beyonce akitumia mwanya wa wakati wanafanya kazi ya pamoja na Beyonce kwa ajili ya MTV, lakini juhudi zake ziligonga mwamba.
Sean-Paul-sean-paul-207569_800_600
Sean Paul ; Huyu jamaa ndiyo anasadikiwa sana kuwa na mahusiano ya siri na Beyonce. Kuna muda walikuwa karibu sana na kufanya mambo mengi pamoja hadi baadaye ketengeneza ngoma ya Baby Boy ya Beyonce pamoja. Ukaribu upo hadi leo na unaweza kuona kwamba hadi marafiki wa Beyonce ni marafiki wa Sean Paul, mtu kama Kerry Rowland ambaye ameipendezesha ngoma ya how deep ya Sean Paul. Sean Paul mwenyewe aliwahi kuulizwa kuhusu hii ishu na alikataa katakata.
worst-marques-houston-2004-large-msg-13070570889
Marquise Huston, huyu jamaa aliwahi kuja Tanzania kipindi flani akiwa na mdogo wake Omarion. Jamaa aliwahi kushikilia bango kwamba aliwahi kuwa na uhusiano na Beyonce akiwa na miaka 17. Baada ya muda kidogo Marquise alipiga kimya mwenyewe.
wyclef
Wyclef Jean, jamaa huyu ambaye pia ni producer aliwasaidia sana wakina Beyonce enzi za Destiny Child kwenye ngoma yao ya kwanza. Katika hizo harakati unaambiwa mtu mzima hakuweka juhudi kwenye kuandaa ngoma peke yake bali pia juhudi ziliwekwa kwenye mtego wa kumnasa Beyonce.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine