
Kuna kitu kinamsumbua Queiroz.
Amewasili Ureno na bosi wake David Gill kufanya mazungumzo ya uhamisho wa winga mpya kutoka kituo cha kukuza vipaji cha Sporting Lisbon, hivyo Queiroz alikuwa anataka kuhakikishiwa kuwa United wanafanya uamuzi mzuri kwa kulipa £17million kwa Luis Carlos Almeida da Cunha aka Nani.
“Carlos alikuwa hotelini in Lisbon,” anakumbuka Pereira, mwenye umri wa miaka 64 na kiongozi wa jopo la maskauti wa kuibua vipaji katika klabu ya Sporting ambaye ana heshima kubwa nchini Ureno kwa kuvumbua vipaji vya nyota kama Luis Figo, Cristiano Ronaldo, Paul Futre na Ricardo Quaresma.
Anaendelea Pereira, “Quieroz alikuwa anataka kujua kuhusu mentality ya Nani na kama angeweza kuhimili presha ya kuichezea United.
“Hakutaka kujua kama alikuwa na miguu mizuri.Alijua kila kitu kuhusu hilo.Alitaka kufahamu kuhusu tabia yake, vipi angeweza kukabiliana na mazingira ya nchi mpya na timu mpya.
“Yalikuwa majukumu mazito kwa Quieroz kwa sababu ulikuwa ni uhamisho wa Euro million 25 na alitaka kuwa uhakika kwa 100%.Nilimtuliza na kumuhakikishia alikuwa anamnunua mchezaji aliyekamilika.”

Masaa kadhaa baadae United walikamilisha uhamisho wa kumsajili kijana wa miaka 20 kwenda Old Trafford, na ukurasa mpya wa maisha ya Luis Nani ukawa umefunguliwa.
0 comments:
Post a Comment