Saturday, March 31, 2012

JOHN BOKO WA AZAM ASTAAFU!

                                                           John Boko wa pili kutoka kulia.

Maji yamemfika shingoni mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya Azam, John Bocco ‘Adebayor’.
Baada ya kuendelea kuzomewa mfululizo na mashabiki wa soka wakati akiwa anaichezea timu ya taifa, John Bocco ameamua kustaafu kuitumikia timu ya taifa ili kuepukana na shida anazozipata kutoka kwa mashabiki wa timu hiyo ya taifa.
Bocco ndio amekuwa mchezaji anayezomewa sana wakati anapoichezea timu ya taifa, jambo ambalo limekuwa likimkosesha raha na amani kwa muda mrefu anapokuwa akiitumikia timu ya taifa lake.
“Nimefikia maamuzi haya baada ya kufikiria sana, nimekuwa nikijitoa kwa hali na mali kulitumikia taifa langu lakini mashabiki wa timu yetu wanaona sifai, hivyo ni bora nijitoe au nistaafu kuichezea timu hiyo ili kuepukana na hilo. Naitakia kila kheri timu yangu ya taifa naipenda na nitaendelea kuipenda siku zote.” – John Bocco

Habari kutoka kwa shaffihdauda.com

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine