Friday, May 11, 2012

VIJANA WA YANGA WATIMBA JANGWANI LEO

WATU wanaosadikiwa kutumwa na wapinzani wa Mwenyekiti wa Yanga, Wakili Lloyd Bahargu Nchunga wamevamia makao makuu ya klabu, kuvuruga Mkutano wa Mwenyekiti huyo na Waandishi wa Habari mchana huu. Watu hao wanadaiwa kufanya vurugu zilizosababisha uharibifu makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam. Nchunga aliitisha mkutano na Waandishi wa Habari wa saa 5:00 asubuhi ya leo, kuelelezea yale yaliyofikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji jana.




0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine