STAA katika tasnia ya filamu Bongo, Yvonne Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’, Julai 6, mwaka huu ndani ya Viwanja vya Sabasaba, Mtoni jijini Dar es Salaam alitimua mbio kumkimbia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.
Monalisa alikuwa kama mtu aliyepandwa na malaria ya ghafla kichwani pale alipomuona ‘laivu’ Rais Kikwete alipokuwa akitembelea mabanda katika viwanja hivyo.
Monalisa akiwa na mama yake, Suzan Lewis ‘Natasha’ pamoja na wasanii wengine waliokuwa kwenye banda la Dk. Rahabu, alitimua mbio baada ya kumuona Rais Kikwete akiwa anatokea mbele yao, akiwa na wapambe wake.
0 comments:
Post a Comment