
MECHI ya
kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya watani wa jadi,
Simba na Yanga itakayopigwa Oktoba 3, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam itachezwa kuanzia Saa 1:00 usiku na kuonyeshwa moja kwa moja na
kituo cha Televisheni cha SuperSport.
Ofisa Habari
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema leo
kwamba hiyo itakuwa moja kati ya mechi tano za Ligi Kuu zilizobatizwa
jina Super Weekend katika mzunguko wa kwanza, ambazo zote zitaonyeshwa
moja kwa moja na SuperSport, zikianza kati ya saa 1:30 jioni na saa 1:00
usiku.

0 comments:
Post a Comment