Thursday, May 10, 2012

BASI LA MURO LATEKETEA KWA MOTO LIKIWA LINATOKEA TABORA KUJA DAR!.


 

Basi lenye namba za usajiri T 820 BEY mali ya kampuni ya Muro Investment lililokuwa likitokea Tabora kuja jijini  Dar es salaam limeteketea kwa moto maeneo ya maseyu Mkoani Morogoro majira ya saa moja usiku wa tarehe 8 may. Basi hilo lililokuwa na abiria 65 lilipata hitilafu kwenye mfumo wake wa umeme uliosababisha shoti iliyoanzisha moto maeneo ya uvungu wa gari hilo, ambapo lilipofika eneo la tukio wananchi waliokuwa chini waliweza kuliona na kupiga kelele ambapo dereva alisimamisha gari hilo, hakuna aliyejeruhiwa wala kufariki kwani abiria wote waliweza kushuka salama baada ya gari hilo kusimama lakini mizigo na mali zote ndani ya gari hilo ziliteketea kwa moto.






0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine