Saturday, September 22, 2012

Demba Ba kuondoka January mwakani


Kocha Mkuu wa Newcastle Alan Pardew amekiri mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal na mfungaji bora wa timu hiyo msimu uliopita Demba Da huenda akaondoka mwezi January kwa kitita cha pauni milioni saba. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na saba amekiri kutokuwa na raha kutokana na kutokuwepo kwenye kikosi cha kwanza cha Newcastle United katika msimu huu.
Pardew amesema kulingana na kifungu ambacho kipo kwenye mkataba wa Demba Ba kinatoa nafasi kwa mshambuliaji huyo kuondoka mwishoni mwa mwezi january kama mambo yataenda tofauti.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine