Monday, September 3, 2012

SIMBA KUKIPIGA NA SOFAPAKA ALHAMISI DAR ES SALAAM


Simba SC

BAADA ya mwezi na ushei wa kuwa kambini nje ya Dar es Salaam, Alhamisi wiki hii wapenzi wa Simba SC watapata fursa ya kuiona tena timu yao ikicheza mbele ya mechi yao, itakapomenyana na waliowahi kuwa mabingwa wa Kenya, Sofapaka FC Uwanja wa Taifa.
Msemaji wa klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga ‘Mr. Liverpool’ akizungumza leo kwamba, mechi hiyo itakuwa ya mwisho kabla ya kucheza na Azam FC, Septemba 11, mwaka huu katika mechi ya Ngao ya Jamii.
Kamwaga alisema kwamba Simba itarejea kesho Dar es Salaam na kuendelea na mazoezi katika Uwanja wa Sigara, Chang’ombe ikisubiri kukipiga na Azam FC.

0 comments:

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine