Tuesday, November 26, 2013

Hatimaye Serikali yabariki TANESCO kupandisha bei za umeme....Naibu waziri asema "atakayeshindwa kumudu gharama hizo, atumie kibatari..."


Naibu Waziri wa umeme, Mh George Simbachawene, amesema kwamba serikali imekubali TANESCO waongeze gharama za umeme kwa 68% kama walivyokuwa wameomba.
  


Simbachawene ameitoa  kauli hiyo wakati akiongea katika kipindi cha Kumepambazuka kupitia Radio One leo asubuhi. 



Amesema kwamba hata kama TANESCO wakiongeza gharama za umeme hadi kufikia Tsh 800 kwa unit bei hiyo ni nafuu kuliko gharama za kununua mafuta ya taa.

Mh Simbachawene ametahadharisha kwamba kama mtu ataona kwamba gharama za umeme ni kubwa, basi akawashe kibatari au akae gizani.

Source: Jamiiforum  via Kumepambazuka, Radio One.

Read more: http://habarizetuleo.blogspot.com/2013/11/hatimaye-serikali-yabariki-tanesco.html#ixzz2lj0RL8aL

3 comments:

Unknown said...

Pata habari za udaku na skendo kwenye mtandao huu udaku bofya neno udaku

Unknown said...

Bofya hapa soma udaku kila siku udaku

Unknown said...

mh kaaaaaaaaz kwel kwel

Post a Comment

 
Design by Uplink Servers Technology | Bloggerized by Kwetu Bongo Online Magazine