Shirikisho
la Vyama vya Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) limetuma Hati ya Uhamisho wa
Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Ayoub Hassan Isiko aliyejiunga na
Mtibwa Sugar akitokea timu ya Bull FC ya nchini humo.
ITC
hiyo ilitumwa jana (Agosti 30 mwaka huu), hivyo kufanya wachezaji ambao
ITC hazijapatikana hadi sasa kubaki wawili tu. Dirisha la usajili wa
wachezaji litafungwa rasmi Septemba 4 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment